Monday, March 16, 2015

WAZIRI MIGIRO AKABIDHI NAKALA ZA KATIBA INAYOPENDEKEZWA KWA WALEMAVU, TAASISI ZA KIDNI NA ASASI ZA KIRAIA

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi  Tanzania (TPSF),  Godfrey Sembeye (kushoto), akipokea nakala ya Katiba inayopendekezwa kutoka kwa Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Asha-Rose Migiro, wakati wa hafla ya utoaji wa katiba hiyo kwa taasisi za serikali na asasi za kiraia iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. 
 Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Asha Rose Migiro akizungumza wakati wa kukabidhi Nakala za katiba iliyopendekezwa kwa taasisi za serikali na asasi za kiraia jijini Dar es Salaam.
 Nakala za katiba iliyopendekezwa.
 Mwenyekiti wa Shirikisho la Watu wenye Ulemavu Tanzania, Amon Mpanju (kushoto) akipokea nakala za Katiba iliyopendekezwa ambayo imeandikwa kwa maandishi ya nukta nundu kutoka kwa Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Asha Rose Migiro. Katikati ni Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Ummy Mwalimu.

Mwenyekiti wa Shirikisho la Watu wenye Ulemavu Tanzania, Amon Mpanju (kushoto) akisoma moja ya nakala ya Katiba iliyopendekezwa iliyoandikwa kwa maandishi ya nukta nundu mara baada ya Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Asha Rose Migiro kumkabidhi. Katikati ni Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Ummy Mwalimu.

Mwenyekiti wa Chama cha Albino Tanzania, Ernest Kimaya akipokea nakala ya Katiba iliyopendekezwa ambayo imeandikwa kwa maandishi makubwa kutoka kwa Waziri wa Sheria na Katiba.
Mwakilishi wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Said Mohamed Lenza akipokea nakala ya Katiba iliyopendekezwa.
Mwakilishi wa Bohora, Zainudin Adamjee akipokea nakala ya Katiba iliyopendekezwa.
Mwakilishi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), ambaye ni Ofisa wa Sheria, Hussein Sengu akipokea nakala ya Katiba iliyopendekezwa.

Friday, February 27, 2015

RITA wazindua mkakati wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi Wilaya ya Kinondoni

Mgeni Rasmi katika Uzinduzi wa Mkakati wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi katika Wilaya ya Kinondoni,Waziri wa Katiba na Sheria,Mh. Dkt. Asha-Rose Migiro akikata utepe kuashiria Uzinduzi wa Mkakati huo,akishirikiana na Mbunge wa Jimbo la Kinondoni,Mh. Iddi Azzan,Meya wa Manispaa ya Kinondoni,Mh. Yussuf Mwenda,Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA),Phillip Saliboko pamoja na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Mhandisi Mussa Natty. Uzinduzi huo umefanyika kwenye Ukumbi wa Shule ya Sekondari Turiani,Magomeni jijini Dar es salaam.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA),Phillip Saliboko akitoa hotuba yake wakati wa Uzinduzi wa Mkakati wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi katika Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam leo,uliofanyika leo Ukumbi wa Shule ya Sekondari Turiani,Magomeni.
Mgeni Rasmi katika Uzinduzi wa Mkakati wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi katika Wilaya ya Kinondoni,Waziri wa Katiba na Sheria,Mh. Dkt. Asha-Rose Migiro akitoa hotuba yake wakati wa Uzinduzi huo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Shule ya Sekondari Turiani,Magomeni jijini Dar es salaam.Wengine pichani toka kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Kinondoni,Mh. Iddi Azzan,Meya wa Manispaa ya Kinondoni,Mh. Yussuf Mwenda pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA),Phillip Saliboko.
Sehemu ya Wajumbe wa Elimu kutoka katika Kata mbali mbali za Wilaya ya Kinondoni,wakifatilia kwa makini hotuba ya Mgeni Rasmi kwenye Uzinduzi wa Mkakati wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi katika Wilaya hiyo.
Waziri wa Katiba na Sheria,Mh. Dkt. Asha-Rose Migiro akikabidhi vyeti vya kuzaliwa kwa baadhi ya wanafunzi kutoka Shule za msingi za Wilaya ya Kinondoni,wakati wa Uzinduzi wa Mkakati wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi katika Wilaya ya Kinondoni.
Meza kuu ikipata picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi hao pamoja na walimu wao.
 Waziri wa Katiba na Sheria,Mh. Dkt. Asha-Rose Migiro (katikati) akimsikiliza Msajili wa Vizazi na Vifo (RITA) Manispaa ya Kinondoni,Mariam Ling'ande (kushoto) wakati akielezea juu ya namna RITA inavyotunza kumbukumbu,wakati wa Uzinduzi wa Mkakati wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi katika Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam leo.Uzinduzi huo umefanyika kwenye Ukumbi wa Shule ya Sekondari Turiani,Magomeni.

Wednesday, June 11, 2014

HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA MUHIMU KWA MAENDELEO - WAZIRI MIGIRO


Mhe. Asha-Rose Migiro ( Mb) Waziri wa Sheria na Masuala ya Katiba, akizungumza wakati wa majadiliano kuhusu mchango wa haki za binadamu na utawala wa sheria katika kuunga mkono juhudi za kitaifa na kimataifa kuelekea upunguzaji wa umaskini na maendeleo endelevu. Waziri Migiro alikuwa miongoni mwa wanajopo wanne walioalikwa na Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhudhuria na kubadilishana mawazo kuhusu nafasi ya haki za binadamu na utawala wa sheria katika ajenda za maendeleo endelevu baada ya 2015. Pamoja na kuzungumzia masuala ya haki za binadamu na utawala bora. Mhe. Waziri alisema Tanzania kupitia Rais wake wa kwanza Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ilianza kutekeleza mipango ya maendeleo ikiwamo ya kupiga vita umaskini, magonjwa na elimu kwa wote, malengo ambayo baadaye Jumuiya ya Kimataifa ilikuja kuyaita Malengo ya Maendeleo ya Millenia MDGs.
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. Jan Eliasson akifungua majadiliano kuhusu mchango wa haki za binadamu na utawala wa sheria katika kuunga mkono juhudi za kitaifa na kimataifa na nafasi yake katika suala zima la maendeleo endelevu baada ya 2015. Naibu Katibu Mkuu alimtambulisha Waziri Migiro kama mtangulizi wake na katika hotuba yake alinukuu baadhi ya maneno ambayo Mhe. Migiro aliwahi kuyazungumza kuhusiana na masuala ya utawala wa sheria wakati huo akiwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.

Muwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Balozi Tuvako Manongi,akifuatilia majadiliano kuhusu mchango wa haki za binadamu na utawala bora katika kusukuma mbele suala zima la upunguzaji wa umaskini na maendeleo endelevu. Wachagizaji wakuu wa majadiliano hayo alikuwa ni Mhe. Asha-Rose Migiro ( Mb) Waziri wa Sheria na Masuala ya Katiba, Bw. Christoph Strasser, Bw. Nicolas Lusian na Bw. Martin Kreutner.
Sehemu ya washiriki wa majadiliano kuhusu mchango wa haki za binadamu na utawala bora katika kuunga mkono juhudi za kitaifa na kimataifa kuelekea upunguzaji wa umaskini na maendeleo endelevu wakimsikiliza Waziri wa Sheria na Masuala ya Katiba Mhe. Asha-Rose Migiro ( Mb).

Na Mwandishi Maalum,   New  York

Waziri wa  Sheria na  Masuala ya Katiba, Asha-Rose  Migiro ( Mb) amesema, ajenda za maendeleo endelevu baada ya 2015 zijielekeze zaidi katika kuyawezesha makundi ya jamii yaliyo katika mazingira magumu.
Ameyasema hayo  siku ya jumanne,wakati alipokuwa akichangia hoja kuhusu  mchango wa  haki za binadamu na  utawala wa sheria katika kuunga mkono juhudi za kitaifa na kimataifa kuelekea  upunguzaji wa umaskini na maendeleo endelevu.

Waziri Migiro alikuwa mmoja wa wanajopo wanne waliojadili hoja hiyo iliyoanzishwa na Naibu  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,  Bw. Jan Eliasson ikiwa ni sehemu ya  mkutano wa siku mbili  ulioandaliwa na  Rais wa Baraza  Kuu la Umoja wa Mataifa na kuwashirikisha wawakilishi kutoka  mataifa mbalimbali.

Pamoja na  kusisitiza  haja na umuhimu wa  ajenda mpya  za maendeleo kujielekeza katika  kuyawezesha makundi hayo ya jamii. Waziri Migiro ameongeza pia kwamba   ni muhimu jumuiya ya kimataifa ikajikita  pia katika kupunguza  pengo la uwiano wa maendeleo kati ya maeneo ya mijini na vijijini.

“ Ni  muhimu kwamba kila sehemu ya jamii ikawezeshwa ili iwe na fursa ya kupata haki,  haki  ya kumiliki mali,  ikiwamo haki  ya  kumiliki na  kurithi ardhi na haki za ajira zenye  ujira sawa kwa kazi sawa” akaeleza Migiro na  kuongeza
Akasema ili hayo na mengineyo yaweze kutekelezwa ni  vema basi  suala la haki za binadamu na utawala wa sheria  vikawa sehemu muhimu ya Ajenda za Maendeleo baada ya 2015 na  vilevile kwa  Malengo  Endelevu ya Maendeleo. 

Akizungumza  kuhusu  utekelezaji wa  Malengo ya Maendeleo ya  Millenia ( MDGs),  utekelezaji wake unaelekea ukingoni.Waziri wa Sheria na Masuala ya Katiba, anasema. Tangu kupitishwa kwa malengo hayo mwaka 2000  nchi nyingi hasa zile zilizokuwa zikikabiliwa na changamoto nyingi za maendeleo  zilijiweka sera na  vipaumbele  katika utekelezaji wa malengo hayo.
“   Tumeshuhudia  nguvu za pamoja katika ngazi ya kitaifa na ya kimataifa katika kuhakikisha kwamba MDGs inakuwa  kiungo cha    ajenda za maendeleo”.  Na  kuongeza kwamba pamoja na  mafanikio  ya kuridhisha katika utekelezaji wa  MDGs hizo, bado  kuna mengi yakutekelezwa”. akasisitiza  Waziri.

Akizungumzi nafasi ya Tanzania katika utekelezaji wa MDGs,  Waziri amesema,  Tanzania imefanikiwa katika utekelezaji wa malengo mengi, ingawa changamoto  kubwa  imebaki katika kulitafutia ufumbuzi pengo   lililopo kati ya  miji na vijiji ili kuhakikisha kwamba watu wote wanakuwa na fursa na haki sawa ya kunufaika  na maendeleo endelevu.
Akasema  anauhakika kwamba  nchi nyingi zinakabilia na changamoto hiyo ya  utofauti mkubwa wa kimaendeleo kati ya  maeneo ya mijini na vijijini. 

“Pengo kati ya miji na vijiji ni eneo moja. lakini  katika utekelezaji wa  MDGS mapengo mengine hujitokeza. Ni kwa sababu hii hapana shaka kuwa  haki za binadamu  na utawala wa sheria ni  viwezeshaji  muhimu vya maendeleo” akasema.

Katika  kusisitiza  umuhimu wa  haki za binadamu na utawala wa sheria katika  kuwapatia wananchi maendeleo endelevu.  Wiziri anatoa mfano kwa kusema ni jambo lisilokubalika kwamba karibu watu   nne  bilioni wanakosa haki zitokanazo na  kutoka utawala wa sheria. Huku watoto saba kati ya kumi katika nchi  zilizonyuma kimaendelo hawana vyeti vya kuzaliwa.

Waziri Migiro anaongeza kuwa “ katika nchi nyingine uwiano kati ya  jaji  na idadi ya watu unasimama katika jaji  moja kwa watu  milioni. Ili hali katika nchi nyingine,  watu wanaendelea kubaguliwa kwa misingi ya  makabila yao,  dini au jinsia. Haya yote Mwenyekiti yanaonyesha umuhimu wa  suala la haki za binadamu na utawala wa sheria kuwa sehemu ya maendeleo endelevu baada ya  2015”.

Tuesday, June 10, 2014

DKT. ASHA-ROSE MIGIRO ALIVYOPOKELEWA KWA FURAHA UMOJA WA MATAIFA

Ili kuwa ni hafla ya aina yake iliyojaa tabasamu, kukumbatiana na maneno ya " welcome back, good to see you again, we have missed you" yakitawala wakati Naibu Katibu Mkuu Mstaafu wa Umoja wa Mataifa Dkt. Asha- Rose Migiro alipofika Ofisini kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon na kisha kukutana na kubadilishana mawazo na Katibu Mkuu mwenyewe wakianza na mazungumzo ya faragha kati yao wawili na kisha kujumuika na wafanyakazi wa Ofisi Binfasi ya Katibu Mkuu na Ofisi Binafsi ya Naibu Katibu Mkuu. baada ya Mazungumzo yake na Katibu Mkuu, Dkt. Migiro pia alikutana na kufanya mazungumzo na Naibu Katibu Mkuu aliyemwachia kijiti Bw. Jan Eliasson.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon akiwa na Dkt. Asha-Rose Migiro ( Mb) Naibu Katibu Mkuu Mstaafu na ambaye sasa ni Waziri wa Sheria na Masuala ya Katiba wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wakati alipotembeleza Katibu Mkuu jana Jumatatu. Hii ni mara ya kwanza kwa Dkt. Migiro kufika Umoja wa Mataifa tangu alipostaafu Unaibu Katibu Mkuu miaka miwili iliyopita. Kabla ya Viongozi hao wawili kupiga picha hii rasmi, walikuwa na mazungumzo ya faragha ( Tete a tete). Waziri Migiro yupo hapa Umoja wa Mataifa kuhudhuria Mkutano ulioitishwa na Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu mchango wa Haki za Binadamu na Utawala wa Sheria katika Maendeleo Endelevu baada ya 2015.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon na timu yake akiwa katika mazungumzo na Dkt. Asha- Rose Migiro ambaye alifuatana na Muwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Balozi Tuvako Manongi na Naibu wake, Balozi Ramadhan Mwinyi. Katika mazungumzo hayo, Katibu Mkuu alisema, Rais Jakaya Mrisho Kikwete amefanya jambo jema kumteua Dkt. Asha-Rose Migiro kwanza kuwa mbunge na kisha kumteua kuwa Waziri anayeshughulikia Sheria na Masuala ya Katiba, akasema uzoefu wake na mchango wake siyo tu kwamba ni muhimu kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bali ni muhimu pia katika Jumuiya ya Kimataifa. Ban Ki Moon alishindwa kuficha hisia zake pale aliposema mbele ya Maofisa wake kwamba siku zote amekuwa akimkumbuka Asha- Rose Migiro na kwamba amefurahi sana kwamba amepata nafasi yakufika Umoja wa Mataifa.
Ban Ki Moon akiagana na Dkt. Asha-Rose Migiro baada ya mazungumzo yao.
Baada ya kuagana na Katibu Mkuu , Naibu Katibu Mkuu Mstaafu Dkt. Asha-Rose Migiro alielekea ofisini kwa Naibu Katibu Mkuu Bw. Jan Eliasson ambako nako kulikuwa na kukaribisha na tabasamu za akina yake. na kisha wakawa na mazungumzo ya faragha.Pichani ni Naibu Katibu Mkuu, Bw. Jan Eliasson akimkaribisha kwa furaha Dkt. Asha- Rose Migiro ofisi kwake kwa mazungumzo.
Wakipata picha ya pamoja.
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Jan Eliasson akiwa na Dkt. Asha- Rose Migiro. Bw. Eliasson alimueleza Naibu Katibu Mkuu Mstaafu kwamba anajitahidi kufuata nyayo zake na kwamba anapenzi makubwa sana na Tanzania na Afrika kwa Ujumla, Bw. Eliasson aliwahi kufanya kazi Tanzania kama mwanadiplomasi chini ya Uongozi wa Rais wa wakati huo wa Sweden Marehemu Olof Palme.
Dkt. Asha- Rose Migiro akiagana na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. Jan Eliasson ( Leo jumanne ) Waziri wa Sheria na Masuala ya Katiba Dkt. Asha- Rose Migiro ( Mb) atakuwa miongoni wa wanajopo ( Panellist) watakaoendesha majadiliano kuhusu mchango wa haki za binadamu na utawala wa sheria katika uungaji mkono juhudi za kitaifa na kimataifa katika kuutokomeza umaskini na maendeleo endelevu. Majadiliano hayo ni sehemu ya mkutano wa siku mbili ambao umeitishwa na Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Bw. John Ashe na kufunguliwa na Katibu Mkuu Ban Ki Moon.Kushoto ni Balozi wa Kudumu wa Umoja wa Mataifa,Balozi Tuvako Manongi
Naibu Katibu Mkuu Mstaafu akipokea shada la Maua kutoka kwa mmoja wa wafanyakazi wa Ofisi Binafsi ya Katibu Mkuu. Ujio wa Dkt Migiro, uliamsha shamra shamra zaina yake kutoka kwa Katibu Mkuu mwenyewe ambaye kila wakati alikuwa akiachia tabasamu pana, Baraza lake la Mawaziri pamoja na wafanyakazi wa ofisi yake Binafsi pamoja na ofisi Binafsi ya Naibu Katibu Mkuu.
" Hili UA zito ngoja tukupokee" ndivyo wanayoelekea kusema Katibu Mkuu Ban Ki Moon na Mkuu wake wa Itifaki.
"welcome back" ndivyo anayosema afisa huyu wakati wakisalimia kwa furana ha Naibu Katibu Mkuu Mstaafu Dkt- Asha-Rose Migiro huku Katibu Mkuu akiangalia kwa furaha.
Ilikuwa ni furaha tupu kwa kweli salamu zikiendelea

Friday, May 10, 2013

KILA LA KHERI JWTZ

TUNAWATIKIA MAFANIKIO MASHUJAA WETU JWTZ WANAPOANZA SAFARI YA KULINDA AMANI JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA KONGO. HIMA HIMA!!!

Thursday, May 9, 2013

WAZIRI MKUU AZINDUA SEMINA YA ALAT


 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Mbunge wa Singida  Mashariki, Tundu Lisu kwenye uwanaj wa ndege wa Kilimanjaro alikowasili  May 8,2013 ili kufungua mkutano Mkuu wa ALAT jijini Arusha, May 9, 2013. Lisu pamoja na wabunge wengine walikwenda Arusha kujionea athari za mlipuko wa bomu kwenye Kanisa Kstoliki la Olasiti.Katikati ni Mbunge wa Igalula  Athumani Mfutakamba.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Hawa Ghasia  (kushoto) na Mwenyekiti wa ALAT , Dr. Didas Masaburi baada  ya kufungua mkutano Mkuu wa   ALAT  kwenye Ukumbi wa Sundown Carnival jijinii Arusha, May 9,2013

UN KUPITIA MPANGO WA UBRAF WAENDESHA SEMINA KWA WATANGAZAJI WA RADIO ZA KIJAMM ZA AFRIKA MASHARIKI


Picha juu na chini ni Mshauri wa Radio Jamii na Mkufunzi wa UNESCO Dar es Salaam Bi. Rose Mwalimu akiendesha majadiliano kuhusu mikakati endelevu itakayowezesha kuihusisha jamii katika program zinazohusu kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi wakati wa warsha iliyofadhiliwa na mpango wa Unified Budget Result Accountability Frame Work (UBRAF) uliochini ya Umoja wa Mataifa.
Mjumbe wa Kongamano lililofadhiliwa na UBRAF lililohusisha Redio za Kijamii za Afrika Mashariki kutoka Kenya Community Media network (KCOMNET) Njuki Githethwa akiwasilisha ripoti ya maendeleo na ufanisi wa mtandao huo ambao unalenga kujenga fursa ya kitaifa ya kuratibu, kulinda na kusaidia sekta ya vyombo vya habari vya kijamii nchini Kenya wakati wa warsha ya siku mbili iliyoratibiwa na mpango wa UBRAF uliochini ya Umoja wa Mataifa iliyofanyika hivi karibuni Terrat Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara.
Picha juu na chini ni Afisa Habari wa Kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Dar es Salaam Bi. Stella Vuzo akizungumzia umuhimu wa kuwa na mikakati madhubuti ya kushirikishana baina ya Waandishi wa habari na Umoja wa mataifa na pia akafafanua mpango mkakati wa Umoja wa mataifa juu ya usalama wa waandishi wa habari pindi wawapo kazini.
Ambapo amewataka ku-share vipindi na habari mbalimbali na Radio ya Umoja wa Mataifa na kuwafanya wao pia kujulikana kimaifa zaidi.
Bw. Jimmy Okello wa COMNETU akitoa tathmini ya ripoti endelevu za Radio za Kijamii nchini Uganda.
Mwakilishi kutoka Mang’elete Community Radio ya nchini Kenya akizungumzia muelekeo na muafaka wa radio za kijamii na kiwango cha mafanikio kilichofikiwa hadi sasa.
Amos Ochieng wa KCOMNET kutoka Kenya akielezea jinsi watangazaji wa Radio za Kijamii za Jumuiya ya Afrika Mashariki wanavyoweza Ku-share habari kupitia mtandao wa kijamii wa pamoja kwa wakati mmoja.
Baadhi ya wadau mbalimbali kutoka tasnia ya habari waliohudhuria semina iliyohusisha Redio za Kijamii iliyofanyika Terrat wilayani Simanjiro mkoani Manyara hivi karibuni kwa udhamini wa Umoja wa Mataifa kupitia Mpango wa UBRAF.

Pichani juu na chini washiriki wa warsha hiyo iliyowakutanisha Watangazaji wa Radio za Kijamii kutoka Kenya, Uganda, Rwanda na Tanzania wakitoa maoni yao ya namna ya kuboresha uandaaji wa vipindi vyao vya Radio za Kijamii sambamba na vikwazo wanavyokumbana navyo katika kazi zao.