Friday, April 26, 2013

AFRIKA IKATAE KUGAWANYWA, KUNYONYWA:TANZANIA


Na Mwandishi Maalum, New York
Baraza  Kuu la  Umoja wa Mataifa,  mwishoni mwa wiki limepitisha kwa kauli moja  Tamko la Kisiasa kuhusu Utatuzi wa  Migogoro  Barani Afrika kwa njia ya  Amani.

Tamko hilo  ambalo ndani yake  linaainsha  na kutambua mchango mkubwa wa   Muungano wa Nchi Huru za Afrika  (OAU) na sasa Muungano wa Afrika ( AU)  katika kuchagiza  na kusimamia  pamoja na mambo mengine, maendeleo ya nchi za Afrika na watu wake,  kupiga vita  umaskini, ujenzi wa utawala bora, demokrasia , haki za  binadamu na utatuzi wa migororo kwa njia za amani.
 Kabla ya kupitishwa kwa Tamko hilo,  Baraza Kuu la Umoja wa  Mataifa,  kwa siku nzima ya Alhamisi na ijumaa asubuhi lilijikita katika  majadiliano  ya mada iliyohusu ‘utatuzi wa migogoro kwa njia ya amani barani afrika’, ikiwa pia ni sehemu na  Baraza hilo kuadhimisha miaka  50   tangu kuanzishwa kwa OAU na baadaye AU.

Miongozi wa viongozi wakuu walioshirikia majadilaino hayo, na ambayo yaliandaliwa na Bw. Vuk Jeremic,   Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, ni Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon,   Rais wa  Equatoria Guinea Theodore Obiang Nguema Mbasogo, Rais Mstaafu wa Burundi Jean Pierre Buyoya  ambaye pia     Mwakilishi  maalum wa Muungano wa Afrika  huko Mali na Sahel,  wakiwamo pia mawaziri  kadhaa wa  Mambo ya Nchi za Nje.

Akiungana na wazungumzaji wengine katika mkutano huo, Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Tuvako Manongi, pamoja na kuainisha sababu na vyanzo vya migogoro Barani Afrika, alisema, Afrika lazima ifikie mahali ikatae kugawanywa.

“Bara la Afrika lina fursa  nyingi,  Afrika inapanda chati. Afrika lazima ikatae kugawanywa, ikatae kudharauliwa na ikatae  kunyonywa” akasema Mwakilishi wa Kudumu, Tuvako Manongi.
Na kubainisha kwamba,  Afrika lazima pia ikatae kutambuliwa kama bara ambalo limejaa migogoro  . “  Huu ni wakati wa  kufufua  upya pan africanism,  hiki ni kipindi cha mwamko mpya wa Afrika. Lazima tufanye kazi kwa pamoja  ili kuwapa matumaini watu wetu” akasisitiza Manongi.

Akasema    wakati tukisherehekea maadhimisho ya miaka 50 wa OAU,  ni  vema kila mmoja wetu akaahidi  upya  kuimarisha ushirikiano kati ya Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika  kama ilivyoainishwa  katika  Sura ya Saba ya Katima ya Umoja  wa Mataifa.

Akatoa mfano kwa kusema  uhusiano huo unapashwa kuendelezwa katika nyanja zote za  usalama na  maendeleo.  Kama ambavyo imeshashuhudiwa  katika   uundwaji wa Jeshi la  Mseto  kati ya Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika   katika Jimbo la Darfur ( UNAMID),  Misheni ya  Muungano wa Afrika huko Somalia, (AMISOM0  na tukio la hivi karibuni la kurejewa na  kuongozewa uwezo mpya Misheni ya Kutuliza Amani katika DRC ( MONUSCO) kulikoendana na kuridhiwa  upelekaji wa Brigedi Maalum inayoundwa na wanajeshi kutoka Tanzania, Afrika ya Kusini na Malawi.

Aidha akasema majadiliano hayo  ya Baraza  Kuu la Umoja wa Mataifa, yamefanyika ikiwa  ni siku chache tu,   tangu kufanyika kwa Mkutano wa Baraza la Usalama la Afrika katika ngazi ya Mawaziri nchini Tanzania,  mkutano ambao pia ulijadili kwa kina pamoja na mambo mengine  hali ya usalama  barani afrika , vyanzo vya migogoro na ufumbuzi wake.

Karibu wazungumzaji wote  wakiwamo wawakilishi wa Marekani na Jumuiya ya Ulaya waliochangia majadialiano hayo ya utanzuaji wa migogoro kwa njia ya amani, licha ya  kutambua, kusifu na kupongeza kazi kubwa ambayo imefanywa na inaendelea kufanywa na   Muungano wa  Afrika na Taasisi za Kikanda katika kipindi cha miaka 50 iliyopita, walisisitiza haja na  umuhimu wa Jumuiya ya Kimataifa kuendeleza ushirikiano wake na Muungano wa Afrika.

Aidha wazungumzaji huo walitambua na kukiri kwamba  Bara la Afrika licha ya  changamoto mbalimbali zikiwamo za migogoro inayoibuka hapa na pale,  imepiga hatua kuubwa za kimaendeleo, kiuchumi na kijamii na kwamba   Bara hilo linastahili kupongezwa na kuendelea kusaidiwa.

Thursday, April 25, 2013

KINANA AKUTANA NA BALOZI WA UBELGIJI NCHINI, LEO

 KATIBU Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kulia) akimkaribisha kwenye Ofisi za Makao Makuu ya CCM, mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam, Balozi wa Ubelgiji hapa nchini, Koen Adam, Balozi huyo alipomtembelea kwa ajili ya salam, leo asubuhi.
 KATIBU Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kulia) akimtambulisha Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro kwa balozi huyo.
 KATIBU Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kulia) akizungumza na Balozi wa Ubelgiji hapa nchini, Koen Adam, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, jijini Dar es Salaam, leo, Aprili 25, 2013. Wapoli kulia ni Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro.
KATIBU Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kulia) akiagana na huyo baada ya mazungumzo yao. Kushoto ni Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro.(Picha zote na Nkoromo Blog

Monday, April 22, 2013

PRESIDENT DR. JAKAYA KIKWETE OPENS AU MINISTERIAL FOR PEACE AND SECURITY IN DAR ES SALAAM

  President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete welcomes former Mozambican President and SADC mediator for Madagascar, Joachim Chissano at Dar es Salaam Serena Hotel during the opening ceremony for the 368th Ministerial Meeting of the Peace and Security Council of the African Union. Looking on isMinister for Foreign Affairs and International Cooperation of the United Republic of Tanzania, Mr Bernard Membe
 President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete delivers his speech during the opening ceremony for the Ministerial Meeting of the Peace and Security of the African Union held in Dar es Salaam this morning.
 A cross section of the delegates and dignitaries who attended the opening ceremony for the Ministerial Meeting of the Peace and Security of the African Union held in Dar es Salaam this morning.
President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete(Centre) in a group picture with some delegates who attended the opening ceremony of the Ministerial Meeting of the Peace and Security of the African Union held in Dar es Salaam this morning.(photo by Freddy Maro.

Saturday, April 13, 2013

RAIS JAKAYA KIKWETE AFUNGUA RASMI BARABARA YA TANGA HOROHORO


 Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akielekea kufungua  barabara ya Tanga – Horohoro ambayo imejengwa kwa kiwango cha lami ikiwa na urefu wa kilomita 65.14 akiwa ameongiozana na  Naibu waziri wa wizara ya ujenzi, Mhe Gerson Lwenge (kulia),  Bw. Daniel Wolde Yohannes, Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Changamoto za Milenia wa Marekani (MCC), Balozi wa Marekani nchini Mhe Alfonso Lenhardt, na mkuu wa mkoa wa Tanga Mhe Chiku Gallawa (kushoto)
Barabara ya Tanga – Horohoro ni sehemu ya barabara inayoiunganisha Tanzania na nchi jirani ya Kenya kupitia mkoa wa Tanga.  Mradi huu umepata msaada wa Serikali ya Marekani kupitia Mfuko wa Changamoto za Milenia (Millennium Challenge Corporation – MCC). Kukamilika kwa barabara hii ni utekelezaji wa azma ya Serikali ya Awamu ya Nne ya kuboresha miundombinu muhimu ya usafiri wa barabara.  Aidha, kukamilika kwa barabara hii kutapanua fursa za kibiashara kati ya Tanzania na Kenya na hivyo kutumia vizuri zaidi fursa za Soko la Pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akifungua rasmi  barabara ya Tanga – Horohoro ambayo imejengwa kwa kiwango cha lami ikiwa na urefu wa kilomita 65.14 akisaidiana na Bw. Daniel Wolde Yohannes, Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Changamoto za Milenia wa Marekani (MCC), Balozi wa Marekani nchini Mhe Alfonso Lenhardt, Barabara hii  ya Tanga – Horohoro ni sehemu ya barabara inayoiunganisha Tanzania na nchi jirani ya Kenya kupitia mkoa wa Tanga.  Mradi huu umepata msaada wa Serikali ya Marekani kupitia Mfuko wa Changamoto za Milenia (Millennium Challenge Corporation – MCC). Kukamilika kwa barabara hii ni utekelezaji wa azma ya Serikali ya Awamu ya Nne ya kuboresha miundombinu muhimu ya usafiri wa barabara.  Aidha, kukamilika kwa barabara hii kutapanua fursa za kibiashara kati ya Tanzania na Kenya na hivyo kutumia vizuri zaidi fursa za Soko la Pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki.
  Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akifurahia baada ya kufungua rasmi  barabara ya Tanga – Horohoro ambayo imejengwa kwa kiwango cha lami ikiwa na urefu wa kilomita 65.14 akiwa  na Bw. Daniel Wolde Yohannes, Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Changamoto za Milenia wa Marekani (MCC), Balozi wa Marekani nchini Mhe Alfonso Lenhardt, Barabara hii  ya Tanga – Horohoro ni sehemu ya barabara inayoiunganisha Tanzania na nchi jirani ya Kenya kupitia mkoa wa Tanga.  Mradi huu umepata msaada wa Serikali ya Marekani kupitia Mfuko wa Changamoto za Milenia (Millennium Challenge Corporation – MCC). Kukamilika kwa barabara hii ni utekelezaji wa azma ya Serikali ya Awamu ya Nne ya kuboresha miundombinu muhimu ya usafiri wa barabara.  Aidha, kukamilika kwa barabara hii kutapanua fursa za kibiashara kati ya Tanzania na Kenya na hivyo kutumia vizuri zaidi fursa za Soko la Pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki.
 Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipanda mti kama kumbukumbu yaq ufunguzi rasmi  barabara ya Tanga – Horohoro ambayo imejengwa kwa kiwango cha lami ikiwa na urefu wa kilomita 65.14. Kuhsorto kwake ni Bw. Daniel Wolde Yohannes, Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Changamoto za Milenia wa Marekani (MCC), na kulia kwake ni  Balozi wa Marekani nchini Mhe Alfonso Lenhardt, Barabara hii  ya Tanga – Horohoro ni sehemu ya barabara inayoiunganisha Tanzania na nchi jirani ya Kenya kupitia mkoa wa Tanga.  Mradi huu umepata msaada wa Serikali ya Marekani kupitia Mfuko wa Changamoto za Milenia (Millennium Challenge Corporation – MCC). Kukamilika kwa barabara hii ni utekelezaji wa azma ya Serikali ya Awamu ya Nne ya kuboresha miundombinu muhimu ya usafiri wa barabara.  Aidha, kukamilika kwa barabara hii kutapanua fursa za kibiashara kati ya Tanzania na Kenya na hivyo kutumia vizuri zaidi fursa za Soko la Pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki.
  Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Bw. Daniel Wolde Yohannes, Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Changamoto za Milenia wa Marekani (MCC) na viongozi na wadau mbalimbali wakikata utepe kwa pamoja kuashiria  uzinduzi  rasmi  wa barabara ya Tanga – Horohoro ambayo imejengwa kwa kiwango cha lami ikiwa na urefu wa kilomita 65.14.  Barabara hii  ya Tanga – Horohoro ni sehemu ya barabara inayoiunganisha Tanzania na nchi jirani ya Kenya kupitia mkoa wa Tanga.  Mradi huu umepata msaada wa Serikali ya Marekani kupitia Mfuko wa Changamoto za Milenia (Millennium Challenge Corporation – MCC). Kukamilika kwa barabara hii ni utekelezaji wa azma ya Serikali ya Awamu ya Nne ya kuboresha miundombinu muhimu ya usafiri wa barabara.  Aidha, kukamilika kwa barabara hii kutapanua fursa za kibiashara kati ya Tanzania na Kenya na hivyo kutumia vizuri zaidi fursa za Soko la Pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Msafara wa Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete ukipita juu ya sehemu ya barabara ya Tanga – Horohoro ambayo imejengwa kwa kiwango cha lami ikiwa na urefu wa kilomita 65.14.  Barabara hii  ya Tanga – Horohoro ni sehemu ya barabara inayoiunganisha Tanzania na nchi jirani ya Kenya kupitia mkoa wa Tanga.  Mradi huu umepata msaada wa Serikali ya Marekani kupitia Mfuko wa Changamoto za Milenia (Millennium Challenge Corporation – MCC). Kukamilika kwa barabara hii ni utekelezaji wa azma ya Serikali ya Awamu ya Nne ya kuboresha miundombinu muhimu ya usafiri wa barabara.  Aidha, kukamilika kwa barabara hii kutapanua fursa za kibiashara kati ya Tanzania na Kenya na hivyo kutumia vizuri zaidi fursa za Soko la Pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki. PICHA NA IKULU

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA AFUNGUA SEMINA YA WENYE ULEMAVU WA NGOZI, LEO


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na baadhi ya washiriki wa semina ya wabunge kuhusu masuala ya Albino baada ya kuifngua kwenye ukumbi wa Msekwa, Bungeni Mjini Dodoma, Aprili13, 2013. Kuliani Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dr.Seif Rashid.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

UMOJA WA MATAIFA WAIDHINISHA UJENZI WA MAJENGO YA TAASISI YA KIMATAIFA -TANZANIA

NA MWANDISHI MAALUM, NEW YORK
Baraza Kuu la  Umoja wa Mataifa    limepitisha  kwa kauli moja Azimio  linalopendekeza kuidhinishwa  kwa hatua zote za   Ujenzi wa  Mradi wa   Taasisi mpya ya Kimataifa  itakayochukua  majukumu  ya   Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda ( ICTR).

Mradi huo wa majengo ya  kisasa, utajengwa katika eneo la LakiLaki Jijini Arusha-Tanzania na   utahusisha Ofisi, vyumba vya  mahakama, na sehemu ya kutunzia nyaraka na kumbukumbu zote za  ICTR.  Eneo hilo la Laki Laki limetolewa na Serikali ya Tanzania kwa Umoja wa Mataifa.

 Baraza    Kuu limepitisha Azimio hilo katika  mkutano wake uliofanyika siku ya Ijumaa ( April 12),mkutano ambao  pia, Baraza lilipokea na kupitisha  maazimio mengine Nane  yaliyowasilishwa na  Kamati ya Tano inayohusika na masuala ya  Utawala na Bajeti katika Umoja wa Mataifa.

Taasisi hiyo mpya  ijukulikanayo kama  Mfumo wa Kimataifa wa Kumalizia  Mashauri Masalia ya iliyokuwa Mahakama ya  Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari au kwa kimombo (  International Residual Mechanism for Criminal Tribunal )- Tawi la Arusha   pamoja na kuhifadhi nyaraka itasimamia kesi za Masalia ambazo zitakuwa bado hazijakamilia baada ya  ICTR kumaliza muda wake mwakani.

Azimio hilo pamoja na mambo mengine, linamtaka Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, kuweka bayana uwajibikaji na uangalizi wa kina katika ujenzi wa mradi ikiwa  ni pamoja na  kuhakikisha kwamba, sheria, taratibu, kanuni na miongozo yote ya  Umoja wa Mataifa     inayohusu manunuzi/ugavi inafuatwa  ipasavyo katika utekelezaji wa mradi huu.

Gharama za mradi zinatarajiwa kuwa kiasi cha dola za kimarekani 8.78 Milioni ( takribani  Sh.14 Bilioni). Fedha hizi zinalipwa na  Nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa. Mradi unatarajiwa kukamilika  kabla ya mwishoni mwa  mwaka 2015.

Aidha kupitia Azimio hilo,  Baraza Kuu  pia limeishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea na jukumu la  kufuatilia kwa karibu mchakato wote unaohusiana na  utekelezaji wa mradi na vilevile katika kuhakikisha kwamba  inashirikiana na Umoja wa Mataifa kufanikisha  Mradi huu.

Halikadharika  kupitia  Azimio hilo, Baraza Kuu limeelezea  kufurahishwa na  maendeleo ya utekelezaji wa mradi hasa kwa kutumia ujuzi wa ndani, (Local knowledge) katika  ubunifu wa majengo (design),   upatikanaji wa  meneja wa mradi na maandalizi ya kina ya gharama za  ujenzi.

Pamoja na pendekezo la  kuidhinishwa kwa hatua za ujenzi wa mradi ,  Baraza pia  kupitia  Azimio hilo , linamtaka KatibuMkuu   kufanya juhudi zote zitakazo pelekea  kupunguza muda wa ujenzi wa mradi .

Katika hatua nyingine,  Baraza  Kuu pia linamtaka Katibu Mkuu  kuanza mazungumzo na Asasi nyingine za Kimataifa ikiwamo ile ya Mahakama Afrika itakayoshughulikia   Haki za Binadamu,  juu ya namna bora ya  kushirikiana katika matumizi ya  miundo mbinu hiyo katika siku za usoni.

Mwaka 2010 Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa, lilipitisha Azimio nambari  1966  la kuanzisha Mfumo wa Kimataifa utakaomalizia Mashauri ya Masalia  kwa zilizokuwa   Mahakama za Kimataifa za Mauaji ya Kimbari  yaliyotokea  nchini Rwanda ( ICTR) na Mauaji ya  halaiki yaliyotokea katika  iliyokuwa Yugoslavia ya Zamani ( ICTY).

Katika azimio hilo Baraza Kuu la Usalama lilibainisha wazi  kwamba  Arusha ndiyo itakuwa makao ya  Tawi la mfuno huo mpya na  The Hague ikiwa ni  makao ya Tawi  jingine.