Monday, March 16, 2015

WAZIRI MIGIRO AKABIDHI NAKALA ZA KATIBA INAYOPENDEKEZWA KWA WALEMAVU, TAASISI ZA KIDNI NA ASASI ZA KIRAIA

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi  Tanzania (TPSF),  Godfrey Sembeye (kushoto), akipokea nakala ya Katiba inayopendekezwa kutoka kwa Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Asha-Rose Migiro, wakati wa hafla ya utoaji wa katiba hiyo kwa taasisi za serikali na asasi za kiraia iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. 
 Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Asha Rose Migiro akizungumza wakati wa kukabidhi Nakala za katiba iliyopendekezwa kwa taasisi za serikali na asasi za kiraia jijini Dar es Salaam.
 Nakala za katiba iliyopendekezwa.
 Mwenyekiti wa Shirikisho la Watu wenye Ulemavu Tanzania, Amon Mpanju (kushoto) akipokea nakala za Katiba iliyopendekezwa ambayo imeandikwa kwa maandishi ya nukta nundu kutoka kwa Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Asha Rose Migiro. Katikati ni Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Ummy Mwalimu.

Mwenyekiti wa Shirikisho la Watu wenye Ulemavu Tanzania, Amon Mpanju (kushoto) akisoma moja ya nakala ya Katiba iliyopendekezwa iliyoandikwa kwa maandishi ya nukta nundu mara baada ya Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Asha Rose Migiro kumkabidhi. Katikati ni Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Ummy Mwalimu.

Mwenyekiti wa Chama cha Albino Tanzania, Ernest Kimaya akipokea nakala ya Katiba iliyopendekezwa ambayo imeandikwa kwa maandishi makubwa kutoka kwa Waziri wa Sheria na Katiba.
Mwakilishi wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Said Mohamed Lenza akipokea nakala ya Katiba iliyopendekezwa.
Mwakilishi wa Bohora, Zainudin Adamjee akipokea nakala ya Katiba iliyopendekezwa.
Mwakilishi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), ambaye ni Ofisa wa Sheria, Hussein Sengu akipokea nakala ya Katiba iliyopendekezwa.

Friday, February 27, 2015

RITA wazindua mkakati wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi Wilaya ya Kinondoni

Mgeni Rasmi katika Uzinduzi wa Mkakati wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi katika Wilaya ya Kinondoni,Waziri wa Katiba na Sheria,Mh. Dkt. Asha-Rose Migiro akikata utepe kuashiria Uzinduzi wa Mkakati huo,akishirikiana na Mbunge wa Jimbo la Kinondoni,Mh. Iddi Azzan,Meya wa Manispaa ya Kinondoni,Mh. Yussuf Mwenda,Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA),Phillip Saliboko pamoja na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Mhandisi Mussa Natty. Uzinduzi huo umefanyika kwenye Ukumbi wa Shule ya Sekondari Turiani,Magomeni jijini Dar es salaam.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA),Phillip Saliboko akitoa hotuba yake wakati wa Uzinduzi wa Mkakati wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi katika Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam leo,uliofanyika leo Ukumbi wa Shule ya Sekondari Turiani,Magomeni.
Mgeni Rasmi katika Uzinduzi wa Mkakati wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi katika Wilaya ya Kinondoni,Waziri wa Katiba na Sheria,Mh. Dkt. Asha-Rose Migiro akitoa hotuba yake wakati wa Uzinduzi huo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Shule ya Sekondari Turiani,Magomeni jijini Dar es salaam.Wengine pichani toka kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Kinondoni,Mh. Iddi Azzan,Meya wa Manispaa ya Kinondoni,Mh. Yussuf Mwenda pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA),Phillip Saliboko.
Sehemu ya Wajumbe wa Elimu kutoka katika Kata mbali mbali za Wilaya ya Kinondoni,wakifatilia kwa makini hotuba ya Mgeni Rasmi kwenye Uzinduzi wa Mkakati wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi katika Wilaya hiyo.
Waziri wa Katiba na Sheria,Mh. Dkt. Asha-Rose Migiro akikabidhi vyeti vya kuzaliwa kwa baadhi ya wanafunzi kutoka Shule za msingi za Wilaya ya Kinondoni,wakati wa Uzinduzi wa Mkakati wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi katika Wilaya ya Kinondoni.
Meza kuu ikipata picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi hao pamoja na walimu wao.
 Waziri wa Katiba na Sheria,Mh. Dkt. Asha-Rose Migiro (katikati) akimsikiliza Msajili wa Vizazi na Vifo (RITA) Manispaa ya Kinondoni,Mariam Ling'ande (kushoto) wakati akielezea juu ya namna RITA inavyotunza kumbukumbu,wakati wa Uzinduzi wa Mkakati wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi katika Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam leo.Uzinduzi huo umefanyika kwenye Ukumbi wa Shule ya Sekondari Turiani,Magomeni.