Tuesday, June 10, 2014

DKT. ASHA-ROSE MIGIRO ALIVYOPOKELEWA KWA FURAHA UMOJA WA MATAIFA

Ili kuwa ni hafla ya aina yake iliyojaa tabasamu, kukumbatiana na maneno ya " welcome back, good to see you again, we have missed you" yakitawala wakati Naibu Katibu Mkuu Mstaafu wa Umoja wa Mataifa Dkt. Asha- Rose Migiro alipofika Ofisini kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon na kisha kukutana na kubadilishana mawazo na Katibu Mkuu mwenyewe wakianza na mazungumzo ya faragha kati yao wawili na kisha kujumuika na wafanyakazi wa Ofisi Binfasi ya Katibu Mkuu na Ofisi Binafsi ya Naibu Katibu Mkuu. baada ya Mazungumzo yake na Katibu Mkuu, Dkt. Migiro pia alikutana na kufanya mazungumzo na Naibu Katibu Mkuu aliyemwachia kijiti Bw. Jan Eliasson.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon akiwa na Dkt. Asha-Rose Migiro ( Mb) Naibu Katibu Mkuu Mstaafu na ambaye sasa ni Waziri wa Sheria na Masuala ya Katiba wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wakati alipotembeleza Katibu Mkuu jana Jumatatu. Hii ni mara ya kwanza kwa Dkt. Migiro kufika Umoja wa Mataifa tangu alipostaafu Unaibu Katibu Mkuu miaka miwili iliyopita. Kabla ya Viongozi hao wawili kupiga picha hii rasmi, walikuwa na mazungumzo ya faragha ( Tete a tete). Waziri Migiro yupo hapa Umoja wa Mataifa kuhudhuria Mkutano ulioitishwa na Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu mchango wa Haki za Binadamu na Utawala wa Sheria katika Maendeleo Endelevu baada ya 2015.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon na timu yake akiwa katika mazungumzo na Dkt. Asha- Rose Migiro ambaye alifuatana na Muwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Balozi Tuvako Manongi na Naibu wake, Balozi Ramadhan Mwinyi. Katika mazungumzo hayo, Katibu Mkuu alisema, Rais Jakaya Mrisho Kikwete amefanya jambo jema kumteua Dkt. Asha-Rose Migiro kwanza kuwa mbunge na kisha kumteua kuwa Waziri anayeshughulikia Sheria na Masuala ya Katiba, akasema uzoefu wake na mchango wake siyo tu kwamba ni muhimu kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bali ni muhimu pia katika Jumuiya ya Kimataifa. Ban Ki Moon alishindwa kuficha hisia zake pale aliposema mbele ya Maofisa wake kwamba siku zote amekuwa akimkumbuka Asha- Rose Migiro na kwamba amefurahi sana kwamba amepata nafasi yakufika Umoja wa Mataifa.
Ban Ki Moon akiagana na Dkt. Asha-Rose Migiro baada ya mazungumzo yao.
Baada ya kuagana na Katibu Mkuu , Naibu Katibu Mkuu Mstaafu Dkt. Asha-Rose Migiro alielekea ofisini kwa Naibu Katibu Mkuu Bw. Jan Eliasson ambako nako kulikuwa na kukaribisha na tabasamu za akina yake. na kisha wakawa na mazungumzo ya faragha.Pichani ni Naibu Katibu Mkuu, Bw. Jan Eliasson akimkaribisha kwa furaha Dkt. Asha- Rose Migiro ofisi kwake kwa mazungumzo.
Wakipata picha ya pamoja.
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Jan Eliasson akiwa na Dkt. Asha- Rose Migiro. Bw. Eliasson alimueleza Naibu Katibu Mkuu Mstaafu kwamba anajitahidi kufuata nyayo zake na kwamba anapenzi makubwa sana na Tanzania na Afrika kwa Ujumla, Bw. Eliasson aliwahi kufanya kazi Tanzania kama mwanadiplomasi chini ya Uongozi wa Rais wa wakati huo wa Sweden Marehemu Olof Palme.
Dkt. Asha- Rose Migiro akiagana na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. Jan Eliasson ( Leo jumanne ) Waziri wa Sheria na Masuala ya Katiba Dkt. Asha- Rose Migiro ( Mb) atakuwa miongoni wa wanajopo ( Panellist) watakaoendesha majadiliano kuhusu mchango wa haki za binadamu na utawala wa sheria katika uungaji mkono juhudi za kitaifa na kimataifa katika kuutokomeza umaskini na maendeleo endelevu. Majadiliano hayo ni sehemu ya mkutano wa siku mbili ambao umeitishwa na Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Bw. John Ashe na kufunguliwa na Katibu Mkuu Ban Ki Moon.Kushoto ni Balozi wa Kudumu wa Umoja wa Mataifa,Balozi Tuvako Manongi
Naibu Katibu Mkuu Mstaafu akipokea shada la Maua kutoka kwa mmoja wa wafanyakazi wa Ofisi Binafsi ya Katibu Mkuu. Ujio wa Dkt Migiro, uliamsha shamra shamra zaina yake kutoka kwa Katibu Mkuu mwenyewe ambaye kila wakati alikuwa akiachia tabasamu pana, Baraza lake la Mawaziri pamoja na wafanyakazi wa ofisi yake Binafsi pamoja na ofisi Binafsi ya Naibu Katibu Mkuu.
" Hili UA zito ngoja tukupokee" ndivyo wanayoelekea kusema Katibu Mkuu Ban Ki Moon na Mkuu wake wa Itifaki.
"welcome back" ndivyo anayosema afisa huyu wakati wakisalimia kwa furana ha Naibu Katibu Mkuu Mstaafu Dkt- Asha-Rose Migiro huku Katibu Mkuu akiangalia kwa furaha.
Ilikuwa ni furaha tupu kwa kweli salamu zikiendelea

0 comments:

Post a Comment